Welcome To POLYHOODTZ




THIS IS NON PROFIT PLATFORM ESTABLISHED SOME YEARS AGO IN TANZANIA it opperates PERPENDICULAR and PARALLEL with the Community. REGARDLESS ON THAT, THIS WEBSITE HAS BEEN BUILT AS DEDICATION FOR THIS PLATFORM BUT ALSO FOR PERSONAL BLOGING.

About POLYHOODTZ

VISION



HISTORIA INATURUDISHA NYUMA WAKATI WA MWAKA 2019 AUGUST 23.

Hapa ni baada ya kupata wazo la kuunda ulingo ambao ungewakutanisha vijana wengi zaidi duniani, kwa lengo la kuchanganua changamoto zinazowakabili, ubunififu wa maisha ya baadae na kujenga muktadha bora kwa ajili manufaa ya wote katika nyanja mbalimbali za kijamii. Alikadhalika sanjari na mawazo hayo tulikuwa na muamko wa kukutanisha vijana katika mwelekeo wa kujenga fikra chanya za kujitegemea, na kujikwamua ka kupiga jeki makundi fulani fulani katika jamii husika. Kwa kuwa mawazo yaliibukia shulenin yakiwa ni mwelekeo na mtazamo wa kitambo kirefu, tulifikiria pia jitihada mbalimbali za kuhakikisha watoto wenzetu wanafanya vizuri, ma hii ilikuwa ni pamoja na kuusisha kampeni mbalimbali ambazo zingechukua nafasi katika muktadha wa masomo. polyhood ni jukwaa lilizoanza na wafuasi takribani 8 na tulikaa mikutano ya mazumgumzo kadhaa, vijana wangu makomredi wanakumbuka, kwa mwendelezo kampeni nyingi tulifanya, na baada ya kuwa tumeondoka shuleni polyhood haikusimama, iliendelea kushika Hatamu. likiwa ni wazo liliogonga kichwa changu kwa mda mrefu. kuipeleka polyhood kimataifa, jitihada hazikulala, ndo maana mpaka hapa tulipo ni kwa misingi ile inayofanya mpaka wewe leo uko hapa unasoma kuhusu sisi. Ukiachilia mbali izo masimulizi hapo juu, kama polyhood tulipenda kuonesha umma juu ya uwezo tulionao kiteknolojia katika kuendelea kukua kisasa kuendana na maendeleo ya sayansi na Teknolojia. tutaambia Rasmi kuhusu mambo mengi Mazuri tuliyowaandalia sio tu vijana wenzetu, bali jamii kwa ujumla maana sisi ni yie na nyie ni sisi. Hivyo basi tunategemeana.

MISSION



Toka kipindi tumeingia ulingoni na kutambulika rasmi tumekuwa tukifanya mambo mengi sana ikiwemo kampeni mashuleni, kuhusu masuala ya kuhamasisha taaluma, kampeni za utunzaji wa mazingira zikiwemo matawi kama ya CoS na BESE AWARDS, hatulali tunaendelea na jitihada ya kampeni za kujitolea na KURUDISHA SHUKRANI kwenye jamii iliyotufikisha hapa. Na kampeni nyingi zilifanyika kama vile za kupelekea mahitaji watu wenye uhitaji kama vile vituo vya watoto yatima n.k. waanzilishi wa Polyhood tulisema hatulali na hatutalala maana ndoto yetu ni kutumikia watu mpaka siku zetu za mwisho. Tunaomba jamii itushike mkono ili tuweze kuwa daraja kwa wengine

User Experience



USIJIULIZE sana kuhusu jina na nembo yetu, maelezo pale kwenye VISSION yanasanifu nembo yetu na maelezo pale kwenye MISSION yanasanifu nembo yetu. kama utakuwa hujaelewa zaidi kuhusu nembo na jina letu usisite kutuandikia IT wetu atakujibu kwa ufasaha mtupu, vilevile tungependa kupata maoni yako. Sanjari na hayo, tunakabirisha watu wote ambao mgependa kujumuika na sisi ama kutushika mkono kwa namna moja ama nyingine.

KARIBU SANA